The House of Favourite Newspapers

MAKONDA ALIVYOWATUNUKU MAGARI MAAFANDE – VIDEO

Sajenti Beatrice akisali baada ya kukabidhiwa gari.

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amewatunuku zawadi mbalimbali yakiwemo magari  maofisa wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kutokana na utendaji wao mzuri kwa jeshi hilo na taifa kwa jumla.

 

Polisi wakitumbuiza katika hafla hiyo.

 

Hafla ya utoaji wa tuzo hizo kwa polisi waliofanya vizuri mwaka 2018 imefanyika katika Ukumbi wa Mlimani City, Dar usiku wa kuamkia leo na kuhudhuriwa na vigogo mbalimbali wa polisi na wadau wengine wa ulinzi na usalama.

 

Makonda (kushoto) na Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es SalaamRPC Mambosasa wakifuatilia hafla hiyo.

Hafla hiyo ya kihistoria kwa jeshi la Polisi na watumishi wake, ilifana kiaina  huku maafande wawili, Staff Sajenti Beatrice Grayson Mmbaga na Konstebo John Joseph Mutashobya wakiibuka na magari mapya kama zawadi kutokana na utendaji wao mzuri katika kutekeleza majukumu yao.

 

Vigogo wa polisi na wageni wengine waalikwa.

Katika utunukiwaji wa zawadi hizo wengine walipatiwa zawadi mbalimbali ikiwemo mifuko ya saruji, mabati, pikipiki na nyinginezo.

 

Wakati wa kupongezana.

Mbali na Makonda, wengine waliohudhuria kwenye hafla hiyo ni Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, makamanda wengine wa jeshi la polisi, maofisa wa jeshi hilo, wasanii wa Bongo Movies na Bongo Fleva na wadau wengine wa ulinzi nchini.

Abdul Misambano akiimba kibao chake cha Asu kwenye hafla hiyo.
Wasanii wa Bongo Movies waliokuwepo. 

 

Wasanii nao wakifurahia. 

 

Mambosasa akimkabidhi Makonda tuzo kwa kulijali jeshi la polisi  Kanda Maalum ya Dar.

 

Sehemu ya wageni waalikwa walivyodamshi.
Gari alilokadhiwa Sajenti Beatrice.
Wanenguaji wa Twanga Pepeta  wakinogesha kama kawa.

 

HABARI/ PICHA: RICHARD BUKOS /GPL

Comments are closed.