Mama wa Mbalamwezi Asimulia Kifo cha Mwanae – Video
KUFUATIA mmoja wa wasanii wa Bongo Fleva wanaounda Kundi la The Mafik, aitwaye ‘Mbalamwezi‘ kufariki dunia usiku wa kuamkia leo, Ijumaa, Agosti 15, 2019, huku chanzo cha kifo chake kikiwa bado hakijajulikana, Global TV inetia nanga nyumbani kwao na marehemu na kuzungumza na wanafamilia.
Akizungumza na Global TV, mama yake mlezi amesimulia kile anachokijua kuhusiana na kifo cha mwanae huyo akidai kuwa amekutwa amepigwa vibaya miguu.
Mwili wa marehemu Mbalamwezi umehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), jijini Dar es Salaam.
Comments are closed.