The House of Favourite Newspapers

Manara Awafananisha Diamond, Kiba Kama Ronaldo & Messi- Video

OFISA Habari wa Klabu ya Simba, Haji Manara, amewakutanisha mahasimu wawili wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz na Ali Kiba.

 

Haji Manara amewakutanisha wasanii hao kwa kuweka video mbili tofauti moja ikiwa ni ya Diamond na nyingine ya mchezaji Ronaldo, zote pamoja katika akaunti yake ya Instagram huku akiwaongelea kila mmoja kwa namna yake anayotambua vipaji vyao.

Manara amemuelezea Diamond kuwa anajituma kwa kupambana zaidi huku akimuita kama Mfalme. Wakati huo huo Manara amesema anampenda Ronaldo lakini Messi anajua mno huku akieleza kuwa Ronaldo anajiongeza zaidi kwa kile anachokifanya jambo ambalo ni sawa na Diamond na Kiba.

 

“Chibu na Kiba wote wana vipaji, ingawa Kiba ana sauti na tone kali zaidi, lakini Chibu amezaliwa kuwa msanii mkubwa na amejiongeza zaidi. Napenda vipaji lakini napenda wanatumia fursa kikamilifu,” alisema Manara.

Comments are closed.