The House of Favourite Newspapers

Manula Aumia Mkono kwa Kukatwa na Kioo katika Chumba cha Kubadilishia Nguo

0
Mlinda mlango wa Simba, Aishi Manula.

Kupitia Ukurasa Rasmi wa Klabu ya  wameripoti kuwa mlinda mlango wao, Aishi Manula ameumia mkono baada ya kukatwa na kioo katika chumba cha kubadilishia nguo (dressing room).

 

“Dakika chache kabla ya kuanza kwa mchezo wetu dhidi ya Geita Gold FC, mlinda mlango wetu Aishi Manula aliumia mkono baada ya kukatwa na kioo katika chumba cha kubadilishia nguo (dressing room).

Manula aliwasili uwanja wa CCM Kirumba akiwa kwenye orodha ya wachezaji wanaocheza mchezo wa leo na baada ya kuingia katika chumba cha kubadilishia nguo akaangukiwa na kioo ambacho kilivunjika baada ya kuegemewa na mashabiki waliokua nje chumba hicho.

Tayari Aishi amepatiwa matibabu na anaendelea vizuri. Tutaendelea kuwajuza hatua kwa hatua ya maendeleo yake.

Leave A Reply