The House of Favourite Newspapers

Mapinduzi Cup kazi inaanza Leo Alhamisi Uwanja wa Amaan, Zanzibar

0

LEO Alhamisi kwa maana ya Desemba 28, 2023, michuano ya Kombe la Mapinduzi inatarajiwa kuanza kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.

Michuano hiyo ambayo bingwa mtetezi ni Mlandege ya Zanzibar, inatarajiwa kufanyika kwenye viwanja viwili, Amaan uliopo Unguja na Gombani kule Pemba.

Kwa msimu huu, jumla ya timu 12 zinatarajiwa kushiriki zikiwa zimepangwa kwenye makundi matatu. Kila kundi linaundwa na timu nne ambapo timu mbili za juu katika makundi, zitafuzu moja kwa moja robo fainali, kisha ‘best looser’ wawili wataungana nao kukamilisha timu nane.

Mchezo wa ufunguzi utakuwa ni mabingwa watetezi, Mlandege watakaocheza dhidi ya URA kutoka Uganda, kisha baadaye, Azam itapambana na Chipukizi.

Jumla ya mechi 25 zinatarajiwa kuchezwa katika michuano hiyo ambapo moja pekee itapigwa Uwanja wa Gombani, hii itakuwa ni ile ya nusu fainali ya kwanza, lakini zingine 24 zilizobaki, zitachezwa Uwanja wa Amaan.

Timu shiriki katika michuano hiyo ni; Azam (Tanzania Bara), URA (Uganda), Chipukizi United (Zanzibar), Mlandege (Zanzibar), Simba (Tanzania Bara), Jamhuri (Zanzibar), APR (Rwanda), Singida Fountain Gate (Tanzania Bara), Yanga (Tanzania Bara), Bandari (Kenya), KVZ (Zanzibar) na Vital’O (Burundi).

 

MAKUNDI

KUNDI A: Azam, URA, Chipukizi United na Mlandege

KUNDI B: Simba, Jamhuri, APR na Singida Fountain Gate

KUNDI C: Yanga, Bandari, KVZ na Vital’O

VIWANJA VITAKAVYOTUMIKA

Amaan (Unguja)

Gombani (Pemba)

RATIBA

DESEMBA 28, 2023

Mlandege         vs      URA

Chipukizi vs      Azam

DESEMBA 29, 2023

Vital’O      vs      Bandari

Jamhuri   vs      Singida

DESEMBA 30, 2023

URA           vs      Chipukizi

Azam        vs      Mlandege

DESEMBA 31, 2023

Vital’O      vs      KVZ

Yanga       vs      Bandari

 

JANUARI 1, 2024

Singida     vs      APR

Jamhuri   vs      Simba

 

JANUARI 2, 2024

URA           vs      Azam

KVZ            vs      Yanga

 

JANUARI 3, 2024

APR           vs      Jamhuri

Simba       vs      Singida

 

JANUARI 4, 2024

Mlandege         vs      Chipukizi

Yanga                 vs      Vital’O

 

JANUARI 5, 2024

KVZ            vs      Bandari

Simba       vs      APR

 

JANUARI 7, 2024

Robo fainali ya kwanza

Robo fainali ya pili

 

JANUARI 8, 2024

Robo fainali ya tatu

Robo fainali ya nne

 

JANUARI 10, 2024

Nusu fainali ya kwanza

Nusu fainali ya pili

 

JANUARI 13, 2024

Fainali

MWANDISHI WETU

Leave A Reply