Mashabiki wa Simba/Kaizer Chiefs Ya Afrika Kusini Wadaka Tiketi za Bure
KAMPUNI ya Global Group kupitia gazeti namba moja la michezo Tanzania, Championi limetoa zawadi za tiketi kwa wateja wake ili waweze kushuhudia mtanange wa leo kati ya Simba na Kaizer Chiefs Ya Afrika Kusini.
Anthon Adam, Mkuu wa Kitengo cha Usambazaji kutoka Global Group amesema kuwa ni kawaida ya kampuni hiyo kurudisha fadhila kwa wasomaji wake kwa kuwapa tiketi hizo ikiwa ni pamoja na zawadi mbalimbali ambazo kampuni hiyo imekuwa ikizitoa.
“Hii ni kwa kawaida yetu kurudisha fadhila kwa wasomaji wetu kwani wamekuwa wakituunga mkono, hivyo ni jambo jema kuwarudishia kile tunachokipata kutoka kwao, kwa kuwa sote ni familia ya Championi. Amesema.
“Wasomaji wetu tuliowakuta wakiwa na nakala ya gazeti la Championi leo Jumamosi Mei 22, 2021 tumewapa tiketi ya kwenye mechi ya Simba dhidi ya Kaizer Chiefs Ya Afrika Kusini. hii imekuwa ni desturi yetu kuwapa tiketi wasomaji wetu wanaokutwa wakiwa na nakala ya gazeti,” aliongeza.