Beyonce Knowles, Mariah Carey, Jenifer Lopez, Celine Dion na mastaa wengine ambao wamefanikiwa kupata watoto mapacha huenda wakashindwa kuzaa tena kwa njia ya kawaida.
Ripoti hii imetolewa na Dr Irfana Koita baada ya Beyonce kutangaza kuwa anatarajia kupata watoto mapacha ambapo mtaalam huyo ameweka wazi kuwa, mastaa wengi wamepata watoto mapacha na jinsi wanavyowapata mapacha hao ni hatari kwani wengi wao hupandikiza.
Mtaalam huyo amesema kuwa hii inakuwa hatari kwa sababu watu wanaopandikiza kupata mapacha hasa kuanzia umri wa miaka 30 mpaka 40 hupata uwezo mdogo wa kupata watoto wengine kwa njia ya kawaida.
Mtaalam huyo alisisitiza kuwa, Beyonce akishajifungua watoto wake hao hatakuwa na uwezo wa kupata wengine kwa njia ya kawaida kitendo ambacho kinawakuta mastaa wengi.
Comments are closed.