The House of Favourite Newspapers

Mastaa Hawa…Ngozi Zao Tata!

0
Jacqueline Wolper

BAADHI ya wasanii wamekuwa wakiwaacha wengi midomo wazi kutokana na mionekano yao ya sasa, wengi wao wakionekana kuwa na ngozi tofauti na walivyokuwa kipindi kifupi cha nyuma, wengine walikuwa weupe kiasi wamekuwa weupe zaidi pia wapo waliokuwa weusi sasa wamekuwa weupe.

Kwenye hili kuna mengi yamekuwa yakisemwa, ikiwemo kutumia vidonge vya kuwang’arisha ama mikorogo ya kisasa ya kupaka ambayo imezagaa inayotengenezwa na watu binafsi, ambayo inauzwa kwa bei ghari inayomtakatisha mtu bila kumgundua kirahisi kama humfahamu vyema.

Katika makala haya, wapo baadhi ya mastaa ambao ukiwaona zamani na sasa utagundua kuwa ngozi zao ni tata;

JACKLINE WOLPER

Kiuhalisia ni mweupe ila sasa kawa mweupe zaidi, jinsi alivyo huwezi kusema kwamba anajichubua ila muonekano wake unazua viulizo kwa mashabiki kwamba undani wa yeye kuwa hivyo ni upi, lakini msimamo wake ni kwamba hiyo ndiyo rangi yake na kinachochangia hivyo ni jinsi anavyojipenda na kuujali muonekano wake.

Staa wa filamu Bongo Yobnesh Yusuph ‘Batuli’

BATULI

Kiuhalisia bishosti huyu ni mweupe ila sasa amekuwa mweupe zaidi kutokana na masuala ya urembo unaochangiwa na vipodozi vya kisasa, naye ni miongoni mwa wasanii ambao mashabiki wake wamekuwa wakikosa majibu ya maswali yao.

TUNDA

Modo huyu naye ni mweupe kiasi, ila wengi wamekuwa wakimjaji muonekano wake wa kipindi cha nyuma na sasa, lakini mwenyewe hajali na wala hajawahi kueleza kwamba anatumia mikorogo ya kumbadilisha rangi yake ya asili.

HAMISA MOBETO

Bibie huyu amezua taflani kutokana na muonekano wake wengi wakimjaji kwamba awali alikuwa maji ya kunde lakini sasa kawa cheupe dawa na kujiuliza kulikoni bila swali hilo kupata jibu, sababu mwenyewe hayupo tayari kukiri hilo.

Amber Lulu

AMBER LULU

Amber naye anaingia katika listi hii ambaye bila kificho aliwahi kutokwa povu kuwa, hata kama anatumia mikorogo hakuna linayemuhusu hilo zaidi ya yeye na maamuzi yake sababu hakuna anayemsaidia kununua.

DAYNA

Awali wakati anaanza kutusua kwenye gemu la Muziki wa Bongo Fleva alikuwa mweusi lakini siku hadi siku rangi yake imeonekana kubadilika na kuwa mweupe, ambapo aliwahi kukiri kujichubua kutokana na mambo ya ujana.

Kajala Masanja.

 

 

KAJALA

Mwanadada huyu kipindi cha nyuma alikuwa maji ya kunde lakini siku hadi siku rangi yake inabadilika kidogokidogo na sasa ameingia kwenye listi ya warembo weupe Bongo.

Vai wa Ukweli

Ni msanii wa filamu ambaye kipindi cha nyuma alikuwa mweupe kiasi lakini sasa amekuwa mweupe kama Mzungu.

SANDRA

Ni zao la Kundi la Kaole jina halisi ni Salma Salmini. Tangu kitambo alikuwa na weupe kidogo, lakini kadri siku zinavyozidi kuyoyoma amezidi kunga’ra na kuwa mweupe pee, jambo linalozua viulizo kwa mashabiki wake.

Leave A Reply