Mawaziri Walivyouaga Mwili Wa Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi, Dar Leo
Mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo walikuwa miongoni mwa umati mkubwa uliojitokeza kuuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ali Hassan ambaye ameagwa Uwanja wa Uhuru jijini Dar.
Waombolezaji hao walionekana kujawa na simanzi kipindi chote cha tukio hilo ambalo liliongozwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Philip Mpango ambapo pia alikuwepo Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na viongozi wengine.