The House of Favourite Newspapers

MBASHA: Wanawake Wananitaka Ila Bado Sijaona

Emmanuel Mbasha

MSANII wa muziki wa Injili Bongo, Emmanuel Mbasha baada ya kukaa muda mrefu akiwa nje ya ndoa, ameweka wazi kuwa wanawake wengi wanamtaka lakini hajaona wa kumuoa kwani anajua akikurupuka yanaweza kumkuta kama yaliyom- kuta huko nyuma.

 

Akizungumza na Showbiz , Mbasha aliyekuwa mume wa Flora alisema kuwa kila siku watu wanamuuliza ataoa lini lakini mwenyewe anaweka wazi kwamba, kwa sasa hana mpango wa kuoa mpaka pale atakapompata mtu sahihi.

 

“Unajua mwanzo nilikurupuka, kwa sasa nitakaa muda mrefu ili nitakayeingia naye kwenye ndoa awe na sifa zote na ikibidi nizeeke naye,” alisema Mbasha.

STORI NA HAMIDA HASSAN ~ GPL

Comments are closed.