The House of Favourite Newspapers

Mbeya Derby Leo Patachimbika

NDANI ya Jiji la Mbeya, leo kuna ‘Mbeya Derby’ ambapo timu za Mbeya City na Tanzania Prisons zitapambana kwenye Uwanja wa Sokoine mjini hapa.

 

Prisons ambao ni wenyeji wa mch­ezo huo, katika michezo mitano iliyo­pita ya derby hiyo, Prisons imeshinda miwili huku Mbeya City wakijitutumua na kuambulia sare mara tatu.

Kocha wa Mbeya City, Ramadhan Nsanzurwimo raia wa Burundi alise­ma kuwa pamoja na uwezo mzuri na rekodi bora za Prisons ni lazima leo wamalize uteja kutokana na maan­dalizi kabambe waliyofanya.

 

“Hatujapata matokeo mazuri kwa kipindi cha hivi karibuni, hii inaonye­sha jinsi gani huwa wanajipanga vizuri kutukabili lakini na sisi hatutakuwa nyuma ni lazima tuhakikishe tunapata matokeo mazuri ambayo ni pointi tatu muhimu,” alisema kocha huyo.

 

Naye Kocha wa Prisons, Abdallah Mohamed alisema: “Tumejipanga kuendeleza rekodi yetu ya kuwachapa Mbeya City japokuwa hatupo kwenye kiwango kizuri tangu kuanza kwa msimu huu lakini tunataka kupata ushindi hiyo kesho (leo).

Comments are closed.