Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Amos Bulaya (CHADEMA) ameruhusiwa kutoka katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alipokuwa amelazwa akitibiwa tangu wiki iliyopita baada ya afya yake kuimarika.
Amesema afya yake imetengemaa lakini amepewa maelekezo kadhaa.
“Kwanza nitapumzika kwa siku 10, hivyo ndivyo nilivyoagizwa na nitatakiwa kurudi tena hospitalini kwa ajili ya kuangaliwa afya yangu zaidi. Kwa sasa nitapumzika kabla ya kurudi jimboni kuendelea na shughuli za maendeleo,” amesema Bulaya.