Mbunge Shigongo Amshukuru Rais Samia kwa Kujenga Lami Buchosa
MBUNGE wa Buchosa, Eric Shigongo amempongeza na kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kitendo cha kutenga fedha ambazo zimewezesha Jimbo la Buchosa kuwa na barabara za lami.
Shigongo ameyasema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari, na kueleza kuwa tangu nchi ilipopata uhuru, Jimbo la Buchosa halijawahi kuwa na barabara za lami lakini Rais Samia amewezesha hilo kuwezekana.
Ameongeza kuwa, licha ya uchumi wa dunia nzima kutetereka kutokana na janga la Corona, bado Rais Samia ameendelea kutekeleza miradi mingi ya maendeleo.