The House of Favourite Newspapers

Mchungaji Eliona Kimaro wa Kanisa la KKKT Kijitonyama Asimamishwa

0
Mchungaji Rev. Dr. Eliona Kimaro.

Mchungaji Rev. Dr. Eliona Kimaro wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Usharika wa Kijitonyama, ni miongoni mwa wachungaji wa kanisa hilo wanaofahamika zaidi. Kanisa la Kijitonyama, ni miongoni mwa makanisa makubwa, watu wa madhehebu mbalimbali wakienda kusali hapo katika ibada zake za jioni, Jumapili na nyingine.
.
Jana, Mchungaji Kimaro akiwa katikati ya semina aliyotarajia kuiongoza kwa wiki mbili, aliwaaga washarika wa Kijitonyama na kusema kwamba amepewa likizo ya siku 60, na ameelezwa kwamba baada ya likizo hiyo hatarudi Kijitonyama.
.
Video hii ya wakati Mchungaji Kimaro anaaga, imesambaa katika kurasa mbalimbali na kuibua maoni tofauti, baadhi ya watu wakihusisha jambo hilo na migogoro ambayo imekuwa ikitokea katika Kanisa hilo na wakipinga Kimaro kuondolewa Kijitonyama.
.
Hata hivyo Mchungaji Kimaro hajaeleza sababu za maamuzi hayo ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania.

Leave A Reply