Mechi Ya Prisons na Yanga Kuchezwa Kesho Samora
Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imetoa taarifa kuwa mechi ya ligi kuu kati ya Tanzania Prisons dhidi ya Yanga iliyotakiwa kuchezwa kesho katika uwanja wa Sokoine Mbeya, itachezwa katika uwanja wa Samora mkoani Iringa
Uongozi wa klabu ya Yanga umepata taarifa hiyo wakati wakijiandaa na safari ya kurejea jijini Dar es salaam baada ya mchezo huo kuahirishwa kutokana na hali ya uwanja wa Sokoine
Timu zote zinapaswa kusafiri kuelekea mkoani Iringa tayari kwa mchezo huo hapo kesho