The House of Favourite Newspapers

Meneja Kampuni Inayojenga SGR Ahukumiwa Jela Miaka 3

0

MENEJA Uwezeshaji wa Kampuni ya Yapi Merkezi inayojenga reli ya kisasa ya (SGR), ambaye ni raia wa Uturuki, Yetkin Gen Mehmen,  amehukumiwa kulipa faini ya Sh.Mil 100 ama kwenda jela miaka mitatu, huku akitaifishwa Dola za Marekani 84, 850 (TSh. milioni 195.91).

 

Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, baada ya mshitakiwa huyo kukiri kosa la kushindwa kutoa tamko ama maelezo ya fedha hizo alizokutwa nazoUwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA).

 

Hakimu Simba amesema kutokana na mshitakiwa kukiri kosa lake mahakama hiyo imemtia hatiani  kwa kukiri kosa hilo.

 

Awali Wakili wa Serikali Mkuu, Shadrack Kimaro, alimsomea mashitaka yake mshitakiwa huyo akidai kuwa Februari 13, 2020, eneo la uwanja wa JNIA, mshitakiwa huyo alikamatwa eneo hilo akiwa na begi la mkononi likiwa na Dola hizo za Marekani..

 

Mshitakiwa alipoulizwa na maofisa wa polisi alishindwa kuzitolea maelezo,  jambo ambalo ni kinyume cha sheria.

Leave A Reply