ALIYEKUWA Meneja wa msanii wa Bongo Fleva, Ruby, aitwaye Hamish ambaye wikiendi iliyopita alifariki dunia baada ya kupata ajali ya gari, amezikwa jana, Desemba 22, 2020, katika Makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam.
Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki, Hamisi Taletale maarufu kama Babu Tale, ni miongoni watu walioshiriki mazishi hayo pamoja na wasanii na waombolezaji wengine.