The House of Favourite Newspapers

Messi Barcelona Hadi 2026

0

STAA wa soka wa kiwango cha Dunia wa Argentina, Lionel Messi amekubali kusalia Barcelona katika mkataba ambao utamuweka kwenye klabu hiyo hadi 2026, Messi amekubali kupunguza nusu ya mshahara wake kwenye mkataba huo mpya.

Messi mwenye umri wa miaka 34, alikuwa mchezaji huru baada ya mkataba wake baada ya msimu kumalizika Juni 30, mwaka huu.

Kwa sasa mchezaji huyo yupo likizo baada ya kushinda Kombe la Copa America na maelezo ya ndani kuhusu kandarasi hiyo hayajakamilishwa.

Kumshawishi Messi kusalia katika klabu hiyo ndilo lililokuwa lengo la Rais mpya wa klabu hiyo, Joan Laporta.

Barca inatazamia makubaliano ya kubadilishana wachezaji yanayohusisha uhamisho wa mshambuliaji Antoine Griezmann na kiungo wa kati wa Atletico Madrid, Saul Niguez ili kupunguza matumizi ya mishahara ya wachezaji.

Wachezaji kama Junior Firpo, Jean Clair Todipo na Carles Alena tayari wameuzwa ili kupunguza matumizi ya klabu hiyo.

Messi alihusishwa na uhamisho wa kuelekea PSG na Manchester City ambapo angekutana tena na mkufunzi wa zamani wa Barcelona, Pep Guardiola.

Messi ndiye mfungaji bora kuwahi kutokea Barcelona akiwa na mabao 672 na kushinda mataji 10 ya La Liga Pia ni mshindi wa taji la Mchezaji Bora wa Dunia (Ballon d’Or) kwa mara sita.

Stori: Sifael Paul

Leave A Reply