The House of Favourite Newspapers

Meya Aliyekamatwa Mwanza Aomba Appointment na Rais Magufuli

0
Meya James Bwire.

Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza, James Bwire ameomba nafasi ya kukutana ana kwa ana  (appointment) na Rais Dkt. John Pombe Magufuli ili amueleze kinachosababisha malumbano na viongozi wenzake jijini hapo.

Bwire amemueleza hayo Rais Magufuli leo eneo la Igogo, alipopata nafasi ya kuwasalimia wananchi wa Mwanza na kutoa salamu za pongezi kwa rais ambaye yupo ziarani mkoani humo kufungua viwanda na miundombinu mbalimbali ya kiuchumi.

Meya James Bwire alikamatwa jana na Jehi la Polisi huku ikidaiwa kuwa amri ya kukamatwa kwake ni agizo la mkuu wa mkoa huo, John Mongella ambapo hata hivyo baadaye aliachiwa huru kwa dhamana.
 
Hata hivyo, Mongella alikana kuamuru kukamatwa kwa kiongozi huyo aliyekuwa akishikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi cha Jiji la Mwanza
 
Bwire alikamatwa katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza wakati wa mapokezi ya Rais John Magufuli ambaye yupo ziarani mkoani humo kwa madai ya kutaka kufanya kitu kibaya kwenye msafara wa rais.
 
Tangu Aprili, Bwire na Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Kiomoni Kibamba wamekuwa katika mgogoro mkubwa, kila upande ukiutuhumu mwingine kuhujumu shughuli za maendeleo.

Aidha, akihutubia katika Viwanja vya Nyakato jana, Rais Magufuli aliwataka Meya James Bwire na viongozi wengine wa mkoa huo (ambao hakuwataja) wamalize malumbano yao ili wawatumikie wananchi.

Leave A Reply