The House of Favourite Newspapers

MEYA KINONDONI AZINDUA KAMPENI YA CHANJO SHINGO YA KIZAZI

Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamini Sitta akizungumza jambo wakati wa uzinduzi wa chanjo ya kuwakinga wasichana dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi (HPV) walio na umri miaka 14.
Baadhi ya wanafunzi waliohudhuria uzinduzi huo.
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Festo Dugange (kulia) akizungumza jambo katika uzinduzi huo.
…Sitta akionyesha chupa yenye chanjo  kama ishara ya uzinduzi rasmi.

MSTAHIKI Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamini Sitta leo Aprili 30 amezindua rasmi chanjo ya kuwakinga wasichana dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi (HPV) walio na umri miaka 14.

 

Sitta amesema tatizo la saratani nchini limekuwa likiongezeka na kukua kila mwaka hivyo kusababisha vifo vya  wagonjwa wengi kupoteza maisha.

 

Ameeleza kuwa Serikali imeanza kutoa chanjo hiyo kwa wasichana wenye umri wa miaka 14 ili kuwakinga dhidi ya virusi vya magonjwa ya zinaa ambayo yanasababisha saratani hiyo.

 

Virusi hivyo vinajulikana kama Human Papilloma Virus (HPV) ambavyo huwaathiri zaidi wanawake. Wataalamu wanasema idadi kubwa ya wanawake wanakufa kutokana na ugonjwa huo kwa sababu ya kutoutambua mapema.

Comments are closed.