MFANYABIASHARA, Krushna Karia (37) Mkazi wa Makoroboi jijini Mwanza, amefutiwa mashtaka yake katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa ambapo alikuwa akikabiliwa na tuhuma za wizi wa vitu mbalimbali vyenye thamani ya Sh milioni 284.8 alivyopewa na Kiwanda cha Cello kwa malengo ya kibiashara.
Mashtaka hayo yamefutwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi ambapo kesi hiyo ilikuwa imekuja kwa ajili ya kutajwa na upande wa mashtaka kuieleza Mahakama kuwa DPP ameamua kutokuendelea na kesi hiyo.