The House of Favourite Newspapers

Miili ya Watu Wawili na Kichwa Kimoja Vyakutwa Hifadhi ya Ruaha

0


Miili ya watu wawili na kichwa cha mtu mmoja vimekutwa kwenye eneo la Hifadhi ya Taifa ya Ruaha Wilayani Mbarali mkoani Mbeya huku vikiwa vimeharibika huku chanzo cha vifo hivyo kikiwa hakijulikani.

 

Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya, Urlich Matei akizungumza na chombo kimoja cha habari mapema hii leo, amethibitisha kukutwa kwa miili na kichwa hicho jana Jumatatu April 26, 2021 na kueleza kwamba polisi wanaendelea na uchunguzi.

 

Kamanda Matei amesema kuwa kwa sasa bado polisi wanandelea na ufuatiliaji wa tukio hilo ili kujua sababu ya vifo hivyo kama ni kutokana na maji ya mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika eneo hilo au mauaji.

Leave A Reply