Mjengo wa Prof. Jay Wapitiwa na Bomoabomoa
Msanii wa muziki, ambaye ni Mbunge wa Mikuni kupitia CHADEMA, Joseph Haule ‘Professa Jay’, yupo matatani kukosa hifadhi baada ya jumba lake la kifahari alilojenga pembezoni mwa Barabara ya Morogoro maeneo ya Mbezi Luis, kuwa miongoni mwa nyumba ambazo zimewekewa alama ya X kuashiria zipo katika hifadhi ya barabara.
Na nyumba ya Mbunge wa Mikumi ni moja ya nyumba ambazo zimewekewa X kuashiria nayo imo miongoni mwa nyumba za kubomolewa.