The House of Favourite Newspapers

Mke, Mume Jela kwa Kuwakeketa Watoto Wao

MAHAKAMA ya Wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara imewahukumu kifungo cha miaka mitano jela, Thadei Parokwa (43) na mke wake Lowema Thadei (34) kwa kuwakeketa watoto wao watatu.

 

Mwendesha mashitaka wa Polisi mahakama ya Wilaya ya Simanjiro, Mkaguzi wa Polisi, Hamilton Moses, alisema shitaka lililowakabili washitakiwa hao kuwa ni ukatili dhidi ya watoto.

 

Amesema kesi hiyo iliripotiwa kituo cha Polisi Orkesmet tarehe Machi 19, mwaka jana baada ya kukamatwa watuhumiwa hao ambao walidaiwa kuwakeketa watoto hao kwa bibi yao aliyekuwa Kitongoji cha Kangala Kijiji cha Lobosireti Wilayani humo.

 

Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Simanjiro, Lugano Kasebele, baada ya kujiridhisha kwa pande hizo mbili, aliwatia hatiani wazazi hao kwenda jela miaka mitano ama faini ya laki sita na fidia ya laki tisa.

Comments are closed.