MKURUGENZI wa Kampuni ya Global Publishers Ltd inayochapisha magazeti ya Uwazi, Amani, Risasi, Ijumaa na Championi, Lydia James Bukumbi, jana alihudhuria mahafali ya mwanaye, Emmanuel Samson, aliyehitimu masomo ya elimu ya awali (chekechea) katika shule ya Elite Sprints, iliyoko Goba jijini Dar.
Katika hafla hiyo, mkurugenzi huyo alimwandalia keki maalum mwanaye yenye ujumbe wa kumpongeza na kumtia moyo ikiwa ni njia ya kushiriki naye furaha hiyo.
“Kupiga hatua moja kwenda nyingine ni jambo la heri na la kumshukuru Mungu, nimefurahi kuona mwanangu anahitimu masomo ya elimu ya awali, namuomba Mungu amjalie afya njema, hekima na busara katika kukua kwake ili mwakani aweze kujiunga na masomo ya elimu ya msingi. Pia ninayo heshima na shukurani za dhati kabisa kwa walimu wa shule hii kwani mafundisho yao yanawalea watoto kielimu na nidhamu bora. Mungu awabariki,” alisema Lydia.