Mkurugenzi Mtendaji Vodacom Anayemaliza Muda Wake Awaanga Wanahabari
MKURUGENZI mkuu wa Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania Plc anayemaliza muda wake Hisham Hendi (kulia) akimtambulisha mkurugenzi mkuu mpya ajaye Sitholizwe Mdlalose (Kushoto) kwa wanahabari waliohudhuria mkutano wa kuwaaga ulioandaliwa bwana Hisham. Kwenye mkutano huo, Hisham aliwashukuru wanahabari kwa ushirikiano waliompa katika kipindi cha uongozi wake, huku akiwaomba kumuunga mkono Sitholizwe katika juhudi zake za kuboresha huduma kwa wateja nchini na hivyo kuiletea maendeleo Tanzania.