The House of Favourite Newspapers

Mmoja wa ‘Wauaji’ wa XXXTentacion Akamatwa

XXXTentacion.

MMOJA wa watu wanaotuhumiwa kumwua mwanamuziki wa Marekani, XXXTentacion, aliyetajwa kwa jina la Dedrick Williams, amekamatwa.

Mwanamuziki huyo aliuawa na watu wanaosemekana walikuwa wawili wakati anaondoka katika duka la pikipiki huko Pompano Beach, Florida, Jumatatu wiki hii.

Watu hao wanasemekana walikuwa wamefika dukani hapo na baadaye kumsubiri wakati anatoka nje na kumwua ambapo walichukua mfuko mdogo kutoka katika gari la marehemu na kuondoka.

Mtuhumiwa Dedrick Williams.

Kamera za usalama zimemwonyesha mtu aliyekuwa amevaa T-shirt nyeupe na ‘kandamili’ za rangi ya machungwa iliyochuja, jambo ambalo polisi wamesema mtuhumiwa huyo ni Dedrick, kwani hata picha yake moja kwenye mtandao wa Facebook imeonyesha ana mavazi hayo.

Mavazi anayotuhumiwa kuyavaa Dedrick siku ya mauaji.

Comments are closed.