The House of Favourite Newspapers

MOOVN DRIVER YATOA MSAADA KITUO CHA WATOTO YATIMA HANANASIFU

Baadhi ya wawakilishi kutoka kampuni ya usafirishai abiria ya Moovn Driver wakishirikiana na  umoja wa madereva wa mtandao (TODA),  wenye T-shirt nyeusi,  wakimkabidhi msaada mwanamama Zainab Bakari ambaye ni mlezi wa kituo cha watoto yatime cha Maunga cha Hananasifu, Kinondoni, Dar.
Wakipeana mkono ikiwa ishara ya kufurahia kukutana na watoto yatima.

KAMPUNI Ya usafirishaji abiria ya Moovn Driver kwa kushirikiana na umoja wa madereva wa mtandao (TODA), leo wametoa msaada wa vyakula na  mavazi kwa kituo cha watoto yatima cha Maunga kilichopo Hananasifu, Kinondoni, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza  katika hafla hiyo, Katibu wa Umoja wa Madereva wa Mtandao (TODA), Fredy Peter,  amesema kuwa msaada huo umelenga kuwapatia nafuu katika mazingira waliyomo na akatoa wito kwa makampuni na taasisi zingine ziige mfano huo kuwasaidia watu wenye mahitaji, hasa watoto wanaoishi kwenye vituo vya mayatima.

 

Comments are closed.