The House of Favourite Newspapers

Moto wa Fiesta Kuwaka Songea Leo

Msanii wa Bongo Fleva, Juma Jux.

BAADA ya moto mkali kuwashwa jijini Mbeya, hatimaye wakazi wa Songea watakuwa na kazi ya kuhakikisha wanauzima moto leo katika Uwanja wa Majimaji ambapo wasanii kama Jux, Ben Pol, Nandy, Maua, Vee Money, Mimi Mars na wengineo watauwasha.

Mmoja wa waratibu wa Fiesta 2017, Fauzia Abdi amejinadi kuwa, wakazi wa Songea wajipange kikamilifu katika suala la burudani kwani wasanii takribani wote waliofanya makamuzi ji­jini Mbeya wa t a u n ­gana na wengine w a p y a kuuwa­s h a moto k a ­t i k a uwan­ja huo wa Maji­maji baada ya ku­kosekana burudani hiyo kwa misimu miwili mfululizo.

Msanii wa Bongo Fleva, Maua Sama.

 

“Kutakuwa na ‘surprise’ kibao hiyo siku maana kuna wasanii hatujawata­ja hapa lakini wasishangae kukutana na mtu ambaye wao hawakumtarajia maana kazi yetu siku zote imekuwa ni kufanya kila liwezekanalo ili tuwabu­rudishe vya kutosha,” alisema Fauzia.

Wasanii wengine ni G-Nako, Stami­na, Roma, Darasa, Aslay, Dogo Janja, Ommy Dim­poz ,Bright na Nchama ambao watapafomu.

Stori: Musa Mateja | Championi Jumamosi

ZARI AVUNJA REKODI! Apokelewa Kama Malkia Mlimani City

Comments are closed.