Mpoto akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa madrasa ya Tidaiya iliyopoTandale.
MWANAMUZIKI wa Muziki wa Asili nchini Tanzania, Mrisho Mpoto maarufu kwa jina la ‘Mjomba’, ambaye pia ni Balozi wa Hifadhi ya Mbuga ya Wanyama ya Ngorongoro, leo ametoa msaada wa mikeka, misahaafu na juzuu kwa watoto wanaolelewa katika kituo cha Mwandaliwa na madrasa ya Tidaiya iliyopoTandale.
Akizungumza na waandishi wa habari wakati akikabidhi zawadi hizo, Mpoto alisema lengo kubwa la kutoa zawadi hizo ni kusaidia malezi ya watoto katika vituo hivyo ili wakue wakiwa katika maadili mazuri.
Mpoto alisema: “Nimeamua kugawana na watoto kidogo nilichojaliwa nacho ili waweze kufurahi lakini pia kuwasaidia katika makuzi hasa kwenye suala zima la kidini na maadili.”
Aidha Mpoto aliongeza kuwa kutokana na mambo mengi yanayoendelea kwa sasa nchini na duniani kote, kuna uwezekano kwa watoto kukua bila misingi mizuri ya dini, heshima na uzalendo kama wasipoandaliwa mazingira mazuri.
Ili kuhakikisha hilo halitokei, Mpoto amesema imekuwa sababu kubwa iliyompelekea kujitolea zawadi hizo ambapo kwa yeye ni kuufungua mwaka 2018 akiwa na thawabu kutoka kwa watoto.
Comments are closed.