SIKU chache baada ya droo ndogo ya Bahati Nasibu ya Shinda Nyumba kufanyika Februari 8 mwaka huu katika Kiwanja chaTaifa cha Burudani cha Dar Live, kilichopo Mbagala Zakhem jijini Dar. Mr Shinda Nyumba, Julius Charles hatimaye leo kaibuka Mtoni Kijichi na kukusanya kuponi kibao za wasomaji.
Mr Shinda Nyumba alitembelea maeneo mbalimbali ya Kijichi, Mbagala Kuu, Mbagala Kibonde Maji, Chemchem na kwingineko ambapo aligawa vipeperushi vya Shinda Nyumba pamoja na kukusanya kuponi kwa wasomaji mbalimbali wa maeneo hayo.
Baadhi ya wasomaji katika droo hiyo walishinda zawadi mbalimbali ikiwemo pikipiki, runinga flat screen, Dinner set, Smart Phones na zawadi nyingine.
Wakizungumza na Kamera ya GPL baadhi ya wasomaji wameshukuru kuanzishwa kwa awamu ya pili ya bahati nasibu hiyo na kila mtu anatamani kushinda.
“Acha na mimi nikate kuponi za Shinda Nyumba nijaribu bahati yangu maana mwaka jana nimeona mwanamke kutoka Iringa akiwa amejishindia nyumba ya awali iliyopo Salasala, hii ya Bunju mimi naihitaji, kila siku nitanunua magazeti ya Global Publishers na kukata kuponi. Alisema mzee shabani Hamisi wa Kijichi.
Na Gabriel Ng’osha/GPL.
Comments are closed.