Chada Boy Kuwapambanisha Gigy Money, Amber Lulu…..
Na GRABRIEL NG`OSHA|RISASA JUMAMOSI| MIKITO NUSUNUSU
MSANII wa Muziki wa Dansi, Chada Boy amepanga kuwapambanisha Video Queen, Amber Lulu na Gigy Money kwenye Valentine Day ili kuona nani mkali. Akizungumza na Mikito Nusunusu, Chada ambaye anatamba na wimbo wa Wauwe alisema ameamua kuwapambanisha wadada hao wa mjini ili GABRIEL NG’OSHA kukata mzizi wa fitina kati yao.
“Valentine’s Day ni siku ya kuzaliwa kwangu, hivyo nimeandaa pati maalumu kwa ajili ya kuwashindanisha Gigy na Amber katika kukata nyonga, pati itafanyikia King D Hotel iliyopo Sinza, jijini Dar, pia atakuwepo msanii Pasha, Tony Star, Hakimu 5 na wengineo,” alisema
Chada
Comments are closed.