Mr Uwazi Amwaga Zawadi Kwa Wasomaji Wake
Msomaji wa Gazeti la Uwazi mkazi wa eneo la Buza-Bakwata akipokea zawadi ya sukari kutoka kwa Mr. Uwazi. Anayeshuhudia kulia ni Ofisa Usambazaji wa Global,Yohana Mkanda.
Wadau wa gazeti la Uwazi wakipozi na Mr. Uwazi huku wakifunua baadhi ya kurasa za gazeti hilo.
Mr. Uwazi akiwa na wasomaji wa gazeti la Uwazi eneo la Buza ambapo baadhi yao wakionesha habari iliyoko kwenye ukurasa wa mbele.
Msomaji wa Uwazi eneo la Mwembe Yanga-Temeke akipokea zawadi baada ya kukutwa na gazeti hilo.
Msomaji wa Uwazi akipozi na Mr. Uwazi kabla ya kupokea zawadi.
Wasomaji wa Uwazi eneo la kituo cha daladala cha Temeke wakifurahia na Mr. Uwazi walipokutwa na gazeti hilo.
Msomaji wa Uwazi akipokea zawadi ya sukari kutoka kwa Mr. Uwazi mara baada ya kukutwa akisoma gazeti hilo.
KATIKA kukelekea kipindi hiki cha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Mr Uwazi leo alitembelea maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam na kugawa zawadi kwa wasomaji wa Gazeti la Uwazi.
Baadhi ya maeneo aliyotembelea ni pamoja na Buza Kwalimboa, Mwembe Yanga, Tandika, Temeke-Sudani na Chang’ombe ambapo aligawa zawadi mbalimbali ikiwemo sukari na kuwarudishia pesa yao waliyonunulia gazeti hilo la Uwazi.
Mr. Uwazi wakati wa utoaji wa zawadi hizo aliambatana na ofisa usambazaji wa Global Publishers, Yohana Mkanda, ambaye wakati Mr Uwazi akigawa zawadi naye alikuwa akipokea maoni mbalimbali yanayohusu gazeti hilo.
Aidha afisa huyo aliwaahidi wasomaji wa gazeti hilo kufanyia kazi maoni yao na kuwaasa kuendelea kulisoma kwani kila Mr Uwazi atakapopita siku za Jumanne akakuta mtu akisoma gazeti hilo, atakuwa akijipatia zawadi.
“Kazi kubwa ya Mr. Uwazi ni kuhakikisha anatoa zawadi kwa wasomaji wa Gazeti la Uwazi mahali popote, hivyo atakapokutwa mpenzi wa gazeti hilo akilisoma atajipatia zawadi papo hapo,” alisema Mkanda.
NA DENIS MTIMA/GPL