The House of Favourite Newspapers

Mrithi wa Omog ana Kazi ya Kupindua Rekodi Hizi

 

LICHA ya kocha Joseph Omog raia wa Cameroon kutimuliwa ndani ya kikosi hicho, lakini takwimu zinaonyesha kuwa ipo kazi kwa mrithi wake kufanya kwa ajili ya kuzipiku takwimu ambazo ameziacha kwenye muda wa mwaka mmoja na miezi sita aliodumu kwenye kikosi hicho.

 

Omog alifungashiwa virago vyake juzi Jumamosi baada ya kikao baina ya pande hizo mbili yaani uongozi wa Simba pamoja na Omog mwenyewe ambapo wote walikubaliana juu ya kusitishwa kwa mkataba wa kocha huyo ambao ulikuwa unaenda hadi tamati ya ligi msimu huu mwezi Mei.

 

Licha ya kutimuliwa huko lakini kocha huyo atakumbukwa kutokana na kuirejesha timu hiyo kwenye michuano ya kimataifa ambayo kwa misimu minne hawakushiriki baada ya kutwaa ubingwa wa FA walioutwaa msimu uliopita kwa kuwafunga Mbao FC ya Mwanza.

 

Lakini pia Omog ilibaki kidogo aifikie rekodi ya kocha Patrick Phiri ya kucheza msimu mzima bila ya kuruhusu kupoteza pointi ambapo yeye kwenye msimu mzima alipoteza mechi nne pekee huku akishinda 21 kwenye mechi 30 za msimu mzima.

Pia kocha huyo ana kijirekodi chake kwenye michuano ya Mapinduzi msimu uliopita ambapo alipoteza mechi moja pekee kati ya sita, mechi ambayo ilimtia doa ni ile ya fainali dhidi ya Azam ambayo walifungwa bao 1-0.

Mchanganuo mzima wa mechi za kimashindano ambazo Omog aliiongoza Simba ni kama ifuatvayo.

 

LIGI KUU

Msimu 2016/17

Mechi 30, kashind a 21, sare 5 na kufungwa 4

Msimu 2017/18

Mechi 11, kashinda 6, sare 5, hajapoteza

Jumla mechi 41, kashinda 27, kafungwa 4 na sare 10

Mapinduzi 2016/17

Kashinda 4, sare 1 na kafungwa 1

Vs Taifa Jang’ombe 2-1

Vs KVZ 1-0

Vs URA 0-0

Vs Jang’ombe Boys 2-0

Vs Yanga 0-0 (penalti 4-2)

Vs Azam 1-0 (kafungwa)

FA

Kashinda mechi 4 kafungwa moja

Msimu wa 2016/17

Vs Polisi 2-0 (ushindi)

Vs Madini 1-0 (ushindi)

Vs Azam 1-0 (ushindi)

Vs Mbao 2-1 (ushindi)

Msimu wa 2017/18

Vs Green 1-1 (kafungwa penalti 4-3)

 

Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Comments are closed.