The House of Favourite Newspapers

Mtanzania atunukiwa tuzo ya heshima ya malkia Elizabeth II

0

Mtanzania Prudencia Paul Kimiti ametunukiwa tuzo ya heshima ya malkia Elizabeth II kutokana na mchango wake mkubwa katika masuala ya jamii katika hafla iliyoongozwa na binti mfalme Anne katika kasri la Windsor nchini Uingereza.

Prudencia Paul Kimiti akikabidhiwa tuzo ya heshima maarufu kama (MBE) na mfalme Charles III. Hii imekuwa kama ndoto kwa mzaliwa huyu wa mkoa wa rukwa,magharibi mwa Tanzania ambaye sasa anaishi uingereza.

Tuzo hiyo ilitokana na mchango wa binti huyo wa Kitanzania katika masuala ya jamii hasa watu weusi na watu wanaotoka bara la Asia waishio nchini Uingereza.

Prudencia kwa sasa anaishi nchini Uingereza, na anafanya kazi kama mkuu wa kitengo cha upelelezi cha mamlaka ya mapato ambapo anahusika na mambo ya forodha na usalama wa mipaka ya Uingereza.Yeye pia ni mwanaharakati wa watu weusi.

Leave A Reply