The House of Favourite Newspapers

Mtoto Amuua Mwenzake Kwa Risasi

0


Mtoto mmoja mwenye umri wa miaka 17, mkazi wa Viwege, Pugu jijini Dar es Salaam, anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kosa la kumpiga risasi na kumuua mtoto mwenzake, Ikhissan Abdilah (10).

 

 

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Ilala, Moses Fundi amesema tukio hilo lilitokea April 2, 2021 ambapo mtoto huyo alikuwa anacheza na mwenzake kisha kumjeruhi na risasi iliyosababisha kupoteza maisha.

 

 

Kamanda Fundi ameongeza kuwa jeshi hilo pia linamshikilia baba wa mtoto huyo, kwa kosa la kushindwa kuihifadhi vyema silaha anayoimiliki na kusababisha mauaji hayo.

Leave A Reply