MTOTO WA ROSE MUHANDO AKABIDHIWA TUZO TATU ZA GOSPEL
Mtoto wa muimbaji nyimbo za Injili, Rose Muhando, Annoint Amani, jana amekabidhiwa tuzo tatu baada ya kufanya vyema kwenye muziki wa injili. Amani alipewa tuzo hizo na wawakilishi kutoka nchi ya Kenya, Uganda na Kongo DR.
Amani amepewa tuzo hizo na Kituo cha Redio Aunthetic cha nchini Rwanda katika hafla maalum iliyofanyika nyumbani kwake Mpiji-Magohe jijini Dar. Hafla hiyo ilihudhuriwa na wageni kutoka nchi mbalimbali zikiwemo Kenya, Rwanda na Congo DR. Tuzo hizo ni kwa ajili ya mwimbaji mwenye vionjo vya kipekee, mwimbaji jasiri na mwimbaji wa tofauti.
Matukio katika picha:
HABARI: ZAINA MALOGO / GPL PICHA : RICHARD BUKOS / GPL
Comments are closed.