NI simanzi, vilio na huzuni vilitawala jana kwa mamia ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Afya ya Sayansi Shirikishi Muhimbili (Muhas), wakati wa kutoa heshima zao za mwisho kwa mwanafunzi mwenzao, Marcus Kahitwa aliyekutwa amefariki dunia chumbani kwake, Mei 19 mwaka huu.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa, marehemu huyo amefariki dunia baada ya kupaliwa na chakula akiwa usingizini, jambo lililosababisha kifo chake.
Comments are closed.