The House of Favourite Newspapers

Mwakinyo: Mfilipino Hafiki Raundi Mbili

BONDIA Mtanzania, Hassan Mwakinyo amesema kuwa mpinzani wake, Arney Tinampay raia wa Ufilipino, hataweza kumaliza hata raundi mbili kwenye pambano lao litakalofanyika Novemba 29 kwenye Uwanja wa Uhuru.

Mwakinyo anatarajia kupanda ulingoni kuchapana na Tinampay anayeshika nafasi ya pili nchini kwao Ufilipino, kwenye pambano la raundi 10 la Super Water kilo 69.

Akizungumza na Kijiwe cha Ndondi, Mwakinyo alisema: “Kwa jinsi nilivyojiandaa na pambano hilo, sidhani kama Tinampay atafika raundi ya pili, kwa sababu mimi napenda sana kumpiga mtu kwa KO, hivyo natarajia kufanya hivyo hata kabla raundi ya pili haijaisha.”

ISSA LIPONDA, Dar es Salaam

Comments are closed.