The House of Favourite Newspapers

Mwakyembe: Tunahitaji Ushindi Katika Soka Dhidi ya Yeyote

0
Waziri wa Michezo, akiongea na wachezaji wa Kilimanjaro Stars katika hafla iliyoandaliwa usiku wa kuamkia leo katika chakula cha pamoja wakati wa kuiaga timu hiyo kuelekea katika mashindano ya vilabu ya Kagame Cup yatakayofanyika nchini Kenya mwezi Desemba mwaka huu.
Wachezaji wa Kilimanjaro Stars wakimisikiliza kwa makini, Mwakyembe.
Wachezaji wakiwa katika maandalizi ya majukumu yao.
Mmoja wa wachezaji wa Kilimanjaro Stars (kulia) akimshukuru waziri Mwakyembe kwa hotuba yake.

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, Harison Mwakyembe, usiku wa kuamkia leo alipata fursa ya kula chakula cha pamoja na wachezaji wa kikosi cha Taifa Taifa Stars ndani ya Sisicape Hotel iliyopo Mbezi Beach jijini Dar es Salaam ambao wanajitayarisha katika mashindano ya Kagame Cup yatakayofanyika mwezi ujao (Seemba) mwaka huu..

Mwakyembe alitumia muda huo kuwaaga wachezaji hao ambapo leo asubuhi wamekwenda nchini Kenya kushiriki katika michuano ya Kagame Cup.

Akiwaaga.  amewataka wayatumie mashindano hayo kuiletea Tanzania heshima ya ubingwa kwani wana kila sababu ya kufanya hivyo kwani Serikali ipo  nao huku akiwata wahakikishe wanashinda kila mchezo ulio mbele yao.

“Ninatambua uwezo wenu ni mkubwa kama mwalimu wemu alivyosema,  hakikisheni mnamtandika kila atakayekuja mbele yenu,  mimi nitakuja mchezo wa pili mkishinda.

“Makipa watatu nawajua wako poa lakini hata ‘straikaz’ wako safi na beki nawajua wachache lakini wapo safi
Hivyo hadi hapo sina wasiwasi na mchezaji yeyote kati yenu zaidi mcheze mkijua Watanzania wapo nyuma yenu na wanahitaji ushindi,” alisema Mwakyembe

Kikosi hicho jana kimeongeza wachezaji watatu wapya ambao ni Yahaya Zaydi (Azam) nafasi ya straika,
Amani Kaita (Nakuru All Stars Kenya) ambaye anacheza nafasi ya kiungo na Ramadhani Kabwili kipa waklabu ya  Yanga ya Dar es Salaam.

(HABARI/PICHA; MUSA MATEJA | GLOBAL PUBLISHERS)

Leave A Reply