The House of Favourite Newspapers

Mzee MajutoAlazwa Tena ICU Muhimbili

MUIGIZAJI nguli nchini Tanzania, Amri Athuman maarufu kama Mzee Majuto amelazwa tena katika chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Jumanne ya wiki hii.

Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Hospitali ya Muhimbili, Aminiel Aligaesha ndiye aliyethibitisha taarifa hizo za kulazwa kwa Mzee Majuto.

 

Hii inakuwa mara ya pili kwa mchekeshaji huyo kulazwa katika Hospitali ya Muhimbili kwani mapema mwaka huu alilazwa Hospitalini hapo kabla ya kupelekwa India kwa matibabu zaidi.

Comments are closed.