Mzee Yusuf Alivyotambulisha Wanamuziki Kundi Jipya Kwa Mbwembwe
Mfalme wa Taarab, Mzee Yusuf usiku wa kuamkia leo akipiga shoo ya nguvu ya kuuaga mwaka 2020 na kuukaribisha mwaka 2021 ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani wa Dar Live alitangaza kuachana rasmi na kundi lake la zamani la Jahazi na Kuanzisha Kundi lake Jipya la Safina. Katika utambulisho wa kundi hilo Mzee alitambulisha wanamuziki atakaokuwa nao kwenye kundi hilo ambapo mbwembwe kibao zilitawala wakati akifanya utambulisho huo.
HABARI/PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS /GPL