The House of Favourite Newspapers

Mzee Yusuf: Tulieni Taarab Inarudi Mahali Pake!

0

MWANAMUZIKI mkubwa wa Taarab hapa Bongo, Mzee Yusuf ‘Mfalme’ amesema kurejea kwake kutaufanya muziki huo kurejea mahali pake kama zamani.

 

Akipiga stori na OVER ZE WEEKEND, Mzee Yusuf amesema, Taarab ilikuwa imelala hivyo kurudi kwake ni kuiamsha tena.

 

“Kwanza nimefurahi jinsi mashabiki walivyonipokea na nimerudi kuwafanyia kazi nzuri na watafurahi. Ushindani siyo sana kwa sababu Taarab ilikuwa imelala hivyo nimerudi kuirudisha mahali pake kama ilivyokuwa zamani,’’ alisema Mzee Yusuf ambaye hivi karibuni alifanya bonge moja la shoo kuashiria kurudi kwake mjini

STORI: HAPPYNESS MASUNGA

Leave A Reply