MTUMISHI wa Mungu Nabii Lucy Natasha kutoka nchini Kenya, ametua nchini leo Alhamisi, Desemba 19, 2019, na kushusha upako katika Tamasha la Shilo lililofanyika katika Kanisa la Mlima wa Moto lililopo Mikocheni ‘B’ jijini Dar es Salaam.
Tamasha hilo linaloaminika kuwa na nguvu kubwa ya Mungu na kujibu maombi ya waumini na wenye matatizo mbalimbali hufanyika kila mwaka Kanisani hapo ambapo mwaka huu linafanyika Desemba hii.
Katika Shilo ya mwaka huu mgeni rasmi ni Nabii wa Kimataifa Mtumishi wa Mungu Natasha kutoka nchini Kenya.
HABARI:NEEMA ADRIAN
PICHA: RICHARD BUKOS /GPL