Nay: Gigy Anatafuta Kiki Kwangu
Staa wa Bongo fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’
Boniphace Ngumije
MKALI wa Ngoma ya Saka Hela, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ ameamua kumfungukia muuza nyago kwenye video za Kibongo, Gift Stanford ‘Gigy Money’ kuwa anatafuta kiki kutumia jina lake katika mahojiano anayofanya na vyombo mbalimbali vya habari.
Video Quen wa Bongo, Gift Stanford ‘Gigy Money’.
Akichonga na Showbiz Xtra, Nay alisema kuwa amekuwa akisikia juu ya Gigy akimsema si chochote kwake na kwamba ni mbahili alishawahi kumlipa elfu ishirini baada ya kumaliza kutengeneza video zake.
“Yaani huyo Gigy anatafuta kiki, namshangaa sana kila sehemu kunisema hovyo, kwanza hatuendani kwa chochote,” alisema Nay.
Hivi karibuni katika mahojiano na Global TV Online, Gigy alisikika akimponda Nay kuwa ni mtu bahili na haitakuja kutokea yupo naye iwe kikazi ama vyovyote kwa kuwa hana hadhi ya kuwa naye.
KUNUNUA NA KUSOMA MAGAZETI YA GLOBAL PUBLISHERS ONLINE, INGIA HAPA==>VODACOM M-PAPER APP
*********
JIUNGE NA SOCIAL MEDIA ZETU
KWA HABARI ZA KITAIFA, KIMATAIFA, MASTAA NA MIKASA YA KUSISIMUA
INSTAGRAM: @Globalpublishers
ERIC SHIGONGO INSTAGRAM: @ericshigongo
TWITTER: @GlobalHabari
FACEBOOK: @GlobalPublishers
SUBSCRIBE YOU TUBE: Global TV Online
GLOBAL TV ONLINE: www.globaltvtz.com
HADITHI ZA KUSISIMUA NA MBINU ZA UJASIRIAMALI, ERIC SHIGONGO FACEBOOK PAGE:@shigongotz