LONDON, England
KAMPUNI ya Nike imetangaza kuwa mpira wa Ordem 4 ndiyo utakaotumika kwenye ligi tatu kubwa barani Ulaya msimu ujao. Kampuni hiyo imetangaza kutumia mpira huo kwenye Ligi Kuu ya England, La Liga na Serie A.
Awali picha ya mpira huo ilivuja, Juni 6, lakini juzi ndiyo kampuni hiyo ilitangaza rasmi kuwa mpira huo utatumika. Mpira huo wenye rangi mbalimbali huku kila ligi kati ya hizo tatu ikiwa na aina ya rangi yake. Kwa mpira wa England wenyewe utakuwa na rangi ya bluu na njano.