The House of Favourite Newspapers

Niyonzima: Tulieni, Simba Hii Bingwa

0
Niyonzima.

KIUNGO wa Simba, Myarwanda, Haruna Niyonzima, amewatu­liza mashabiki wa timu hiyo, akidai licha ya matokeo ya sare waliyoyatoa dhidi ya Mbao, anaamini timu hiyo itatwaa ub­ingwa mwishoni mwa msimu.

Simba ambayo ina pointi nane katika msi­mamo wa ligi, imetoa sare michezo miwili na kushinda michezo miwili kati ya michezo minne iliyocheza.

Akizungumza na Championi Jumatatu, Niyonzima amese­ma kuwa, kikosi chao kipo vizuri na wanaamini watafani­kiwa kutwaa ubingwa licha ya upinzani mkubwa wanaokumbana nao.

“Kikosi cha Simba kwa ujumla kipo vizuri kwani hata mabao tuliyofun­gwa na Mbao yalikuwa ya kushtukiza, tulimi­liki mpira kwa asil­imia 90 ya mchezo na kilichotokea ni bahati tu ambayo haikuwa yetu.

“Kwa ubora wa kikosi chetu kilivyo, nina imani ya kuweza kutwaa ubingwa msimu huu, kikubwa zaidi ni ku­weza kujituma uwanjani,” alisema Niyonzima.

Khadija Mngwai, Dar es Salaam.

SIRI Imefichuka Baada ya Kushushwa kwa Bilionea Yanga wa Kulipa Mishahara

Leave A Reply