NJENDANI YA EFM REDIO YAWAFIKIA WAKAZI WA KINONDONI
Efm redio imewafikia wakazi wa Kinondoni siku ya leo ya tarehe 22/09/2017, kwa kupitia tamasha lake la Njendani lililofanyika katika uwanja wa Biafra – Kinondoni, ambapo watangazaji wa Kipindi cha Joto la Asubuhi, sports HQ, Uhondo na Ladha 3600 wakitangaza moja kwa moja katika kiwanja hicho pamoja na burudani mbalimbali za muziki ikiambapata na kampeni ya kuchangia damu ilioongozwa na Mpango wa Damu salama katika kuokoa maisha ya wagonjwa waliofanyiwa upasuaji wa moyo.