The House of Favourite Newspapers

ESHA KUMWANIKA MWANAYE LEO

0
Esha Buheti na mwanaye.

MSANII wa filamu za Kibongo, Esha Buheti leo anatarajia kumwanika mwanaye kwa ndugu na marafiki ambapo atamfanyia sherehe ya nguvu.

Akistorisha na Risasi Jumamosi, Esha ameamua kufanya sherehe hiyo pamoja na kumshukuru Mungu kwa kumjalia kujifungua salama na kumlinda mwanaye huyo ambapo itafanyika nyumbani kwake Kijitonyama, Dar na itahudhuriwa na watu mbalimbali wakiwemo wasanii wenzake.

“Jumamosi (leo) ninatarajia kumtoa mwanangu rasmi hivyo sherehe itafanyika hapa nyumbani kwangu, unajua nafanya hivi kwa ajili ya kumshukuru Mungu na kufurahia zawadi hii aliyotupatia katika familia yetu na siyo kwa ajili ya kujionesha,” alisema Esha.

STORI: GLADNESS MALLYA | RISASI JUMAMOSI

TAMTHILIA YA SHEVOLA

Leave A Reply