The House of Favourite Newspapers

NMB yamwaga misaada kwa timu za jeshi, wanajeshi watoa tambo

Kaimu Mkuu wa Wateja Wadogo kutoka Benki ya NMB, Salie Mlay (kushoto)  akimkabidhi jezi  Kanali Damian M. Majare (katikati). Anayeshuhudia ni Erasmus Bwegoge Mkurugenzi wa Utimamu wa Mwili, Michezo na Utamaduni wa JWTZ. 

 
Timu za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) zimepokea msaada wa vifaa vya michezo kwa ajili ya kuboresha timu zao mbalimbali zinazoshiriki katika Ligi Kuu Bara na michuano ya mbalimbali ya majeshi.
 
Msaada huo wenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 10 umetolewa na Benki ya NMB Tanzania, leo Jumatatu jijini Dar es Salaam na kupokelewa na Kanali Damian M. Majare ambaye ni Kaimu Mwenyekiti wa Kanda ya Ngome.
 

Akizungumza katika hafla hiyo, Kanali Damian M. Majare alisema vifaa hivyo vitawawezesha kujiimarisha kukabili michuano ya majeshi inayotarajiwa kuanza mapema mwakani.
 
Kwa upande wake, Kanali Erasmus Bwegoge ambaye ni Mkurugenzi wa Utimamu wa Mwili, Michezo na Utamaduni kutoka JWTZ amesema timu zitakazonufaika na msaada huo ni pamoja na timu za Ruvu Shooting, JKT Tanzania, Green Warriors, Mlale JKT ya Songea, Mgambo Shooting na baadhi ya timu ambazo zinashiriki Ligi Daraja la Kwanza.

Naye Kaimu Mkuu wa Wateja Wadogo kutoka Benki ya NMB, ambao ndiyo wametoa msaada huo, Salie Mlay amesema kuwa wanalenga kuona Timu za JWTZ zikiongeza mwamko katika mashindano mbalimbali hususan mashindano ya majeshi ili waweze kuliwakilisha taifa kikamilifu.

 

Comments are closed.